Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mchakato uvunjaji Jiji la Dar wahojiwa bungeni
Habari za Siasa

Mchakato uvunjaji Jiji la Dar wahojiwa bungeni

Muonekano wa jiji la Dar es Salaam
Spread the love

 

SERIKALI imeombwa kupitia upya mchakato wa ugawaji mali za iliyokuwa Jiji la Dar es Salaam, baada ya kuvunjwa na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Ombi hilo limetolewa leo Alhamisi, tarehe 24 Juni 2021 na Mbunge wa Mbagala mkoani Dar es Salaam(CCM), Abdallah Chaurembo, katika kipindi cha maswali na majibu, bungeni jijini Dodoma.

Mbunge huyo wa Mbagala amedai kuwa, mchakato wa ugawaji mali hizo haukuwashirikisha wabunge na mabaraza ya madiwani ya mkoa huo, hali iliyopelekea mgawo wake kutokuwa sawa.

“Kwa kuwa mgawanyo wa mali wa iliyokuwa Jiji la Dar es Salaam, haukushirikisha wadau wakiwepo wabunge na mabaraza ya madiwani. Je, Serikali haioni iko haja ya kui-review (kupitia) ule mgawo, hasa katika mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu?” Amehoji Chaurembo.

Abdallah Chaurembo, Mbunge wa Mbagala (CCM)

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi, David Silinde, amesema Serikali italifanyia kazi ombi hilo, ili kubaini kama mchakato huo haukushirikisha wadau, kwa ajili ya kuangalia namna ya kuwashirikisha.

“Jambo alilolileta mbunge ni kubwa, inahitaji tufuatilie na tujiridhishe. Kwa sababu nina imani kila jambo linapofanyika kunakuwa na muhutasari, ambao huwa unaandikwa na vikao na idadi ya watu waliohudhuria,” amesema Silinde na kuongeza:

“Endapo jambo hili halikufanyika, basi ninaamini Tamisemi itazingatia namna bora kabisa, itakayosaidia jambo hili kufanyika kwa ukamilifu. Tutalipokea na kufanyia marekebisho.”

Jiji la Dar es Salaam lilivunjwa na Magufuli tarehe 24 Februari mwaka huu, ambapo aliipandisha hadhi iliyokuwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, kuwa Jiji la Dar es Salaam.

Magufuli aliyefariki dunia akiwa madarakani tarehe 17 Machi 2021, alilivunja jiji hilo kwa maelezo kwamba, waliokuwa viongozi wake hawakuwa na eneo wanalowawakilisha wananchi, licha ya kutengenewa bajeti na posho, kitendo kilichosababisha matumizi mabaya ya fedha za umma.

Katika hatua hiyo, waliokuwa watumishi wa jiji hilo, walihamishiwa katika vituo vingine vya kazi, huku mgawanyo wa mali na madeni ya yaliyokuwa ya jiji hilo, ulifanyika kwa mujibu wa sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!