Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rungwe apeleka sera ya ‘ubwabwa’ Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Rungwe apeleka sera ya ‘ubwabwa’ Ikulu

Spread the love

 

HASHIMU Rungwe, aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania, kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) mwaka 2020, ameshauri Rais Samia Suluhu Hassan aifanyie kazi sera yake ya kugawa chakula bure kwa wananchi (ubwabwa).

Rungwe ametaja maeneo muhimu ya utekelezwaji wa sera hiyo aliyoinadi wakati wa kampeni za uchaguzi huo, ni shuleni na hospitalini.

Mwanasiasa huyo ametoa ombi hilo leo Jumatano, tarehe 23 Juni 2021, alipozungumza na MwanaHALISI Online, ofisi kwake Makumbusho, Dar es Salaam.

Amemshauri Rasi Samia aandae mkakati utakaowezesha ajenda hiyo kutekelezwa, ili kuwasaidia wanafunzi kukabiliana na njaa shuleni na wagonjwa wanaolazwa hospitali.

 “Serikali ipange mpango wa kutoa bure chakula hospitalini kwa wagonjwa wanaolazwa na wanafunzi wapate mlo wa chakula.  Sio wang’anganie kusoma wakiwa na njaa, wahakikishe wanafunzi wanaokwenda shule, wanapata chakula kama inavyofanywa na shule binafsi,” amesema Rungwe.

Katika kampeni zake za Uchaguzi Mkuu wa 2020, Rungwe alijizolea umaarufu kwa sera yake ya kugawa ‘ubwabwa’ bure shuleni na hospitalini.

Katika kampeni hizo, Rungwe alisema serikali yake itatenga fedha kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!