Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwigulu abainisha mkakati kupunguza foleni Dar, barabara mikoani
Habari za Siasa

Dk. Mwigulu abainisha mkakati kupunguza foleni Dar, barabara mikoani

Spread the love

 

WAZIRI wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba, amebainisha mikakati mbalimbali ya kupunguza msongamano jijini Dar es Salaam ni ukarabati wa barabara kilomita 138.5. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Dk. Mwigulu, amesema hayo leo Alhamisi, tarehe 10 Juni 2021, wakati akiwasilisha bungeni jijini Dodoma, taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022.

Amesema, Serikali itaendelea na ujenzi na ukarabati wa barabara za kupunguza msongamano za Jijini Dar es Salaam (km 138.5).

“…pamoja na barabara za mikoa, kuboresha miundombinu ya mabasi yaendayo haraka kwa awamu zote nne, ujenzi wa barabara za juu (Flyover) jijini Dar es Salaam,” amesema Dk. Mwigulu.

Pia, amesema, uboreshaji wa barabara za mzunguko katika Jiji la Dodoma pamoja na barabara za vijijini na mijini kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura).

“Vilevile, Serikali itaendelea na ujenzi wa madaraja makubwa yakiwemo madaraja ya New Wami (Pwani), Kitengule (Kagera), Kirumi (Mara) na Mkenda (Ruvuma),” amesema

Waziri huyo amesema, kipaumbele kitawekwa katika barabara za lami, zinazofungua fursa za kiuchumi ambazo ni: barabara za Kidatu – Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo – Lumecha/Songea (km 499); Lukuyufusi – Mkenda (km 122.5); Ifakara – Kihansi – Mlimba – Madeke – Kibena (km 220); Tabora – Ipole – Koga – Mpanda (km 365.36) na barabara ya Makutano – Natta – Mugumu/Loliondo – Mto wa Mbu (km 235);

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Zingine ni; Manyoni – Itigi – Tabora (km 259.75); Handeni– Kiberashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (Km 460); Dodoma – Mtera – Iringa (km 273.3); Dodoma – Babati (km 243.8); Mbeya – Chunya – Makongolosi – Rungwa – Itigi – Mkiwa (km 528) na Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora (km 389.7);

Pia, barabara ya Mtwara – Newala – Masasi (km 210); Barabara ya Masasi – Songea – Mbamba Bay (km 343.2); Barabara ya Nzega – Tabora (km 289.7); Barabara ya Msimba – Ruaha Mbuyuni/Ikokoto Mafinga (km 234.8); Igawa – Songwe –Tunduma na Mchepuo wa Mbeya (km 273.5); na Makambako – Songea na Mchepuo wa Songea (km 295).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!