Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Mzanzibari kuwania urais TFF
MichezoTangulizi

Mzanzibari kuwania urais TFF

Ally Saleh 'Alberto'
Spread the love

 

MWANASOKA maarufu nchini, Ally Salehe ‘Alberto,’ amejitosa katika mbio za kuwania urais ndani ya shirikisho la soka nchini (TFF). Anaripoti Saed Kubenea ….(endelea).

Uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo – Tanzania Football Federation – umepangwa kufanyika tarehe 7 Agosti mwaka huu, jijini Tanga.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, mwanamichezo huyo amesema, ameamua kujitosa katika kinyang’anyiro hicho, ili kuendeleza mchezo wa soka nchini na kusaidia Zanzibar, kupata uanachama wake katika mashirikisho ya Soka ya CAF na FIFA.

Amesema, “ninakwenda kuendesha na kuendeleza mchezo wa soka. Ninakwenda TFF kusimamia mchezo wa soka, ambao ni kipenzi cha wengi. Ninakwenda TFF, ili kukuza vipaji na kusaidia timu ya taifa, Taifa Stars ifanye vizuri kwenye michuano ya kimataifa.”

Kujitosa kwa Ally Salehe ambaye kitaaluma ni mwanasheria, mwandishi wa habari za michezo na aliyewahi kuwa mtangazaji wa shirika la utangazaji la Uingereza (BBC) na wakala wa kimataifa wa wachezaji wa soka anayetambuliwa na FIFA na CAF, kunatajwa na wachambuzi wa soka, kuwa kumechochea ndimu kwenye uchaguzi huo.

 

Kwa takribani miaka 40 sasa, Zanzibar imekuwa ikililia uanachama wake FIFA na CAF. Miaka 10 iliyopita, wakati wa uongozi wa Ledga Tenga na baadaye Jamal Malinzi, ndipo Zanzibar ilifanikiwa kuwa mwanachama wa muda wa CAF.

Kwa mujibu wa Ally Salehe mwenyewe, amepanga kesho Ijumaa, kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo na Jumamosi mchana anaweza kurejesha, akiwa tayari ametimiza masharti yote yanayotakiwa.

Mpaka sasa, ni wagombea wawili pekee, waliojitokeza kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya urais ndani ya TFF. Wagombea hao, ni Wallace Karia, rais anayetetea nafasi yake na Oscar Oscar, ambaye ni mfanyakazi wa kituo cha radio cha E-FM, jijini Dar es Salaam.

Ikiwa mwanasoka huyo mahiri nchini, atajitosa kuwania nafasi hiyo, basi hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Mzanzibari, kugombea nafasi ya urais wa TFF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

error: Content is protected !!