Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Tanzania yasisitiza wananchi kujikinga na corona
Afya

Tanzania yasisitiza wananchi kujikinga na corona

Mkurugenzi wa Idara ya Kinga wa wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto, Dk. Leonard Subi
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesisitiza miongozo yote iliyotolewa kwa umma kujikinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya corona (COVID – 19), izingatiwe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mkurugenzi wa Idara ya Kinga wa wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto, Dk. Leonard Subi amesema, Tanzania ni salama.

Hata hivyo, Dk. Subi amesema, bado kuna tishio la maambukizi ya virusi hivyo duniani, ni muhimu kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga.

Dk. Subi amesema hayo leo Jumanne, tarehe 8 Juni 2021, alipohojiwa na moja ya chombo cha habari jijini Dodoma ni hatua gani Tanzania inaendelea kuzichukua kuhakikisha jamii inakingwa dhidi ya wimbi jipya la maambukizi ya COVID-19.

“Tanzania tupo salama, lakini tunatakiwa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi hayo ambayo kwa takriban mwaka na nusu sasa bado yanaikabili dunia.”

“Wizara kazi yetu ni kuendelea kihimiza wananchi kujikinga dhidi ya COVID -19, tuendelee kuchukua tahadhari,” amesema Dk. Subi.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

“Tuliona katika wimbi la kwanza 2020 wananchi waliitika wito wa kunawa mikono, kuvaa barakoa, kukaa umbali, kufanya mazoezi, lishe bora na masuala mengineyo,” amesema.

Dk. Subi amesema, “tunataka kusisitiza kinachotokea Afrika maambukizi yanaongezeka na baadhi ya wakuu wa nchi wanatoa matamko kama tulivyomsikia Rais wa Uganda, Yoweri Mseven na sisi Tanzania tumekuwa na mwingiliano na uhusiano mwema na nchi jirani.

“Watanzania kinga ni bora kuliko tiba tusije tukasubiri kuingia kwenye mitungi ya oksijeni, tuendelee kujikinga. Hali ni shwari hata Rais Samia Suluhu Hassan, anachukua tahadhari kujikinga na maambukizi akikutana na watu mbalimbali,” amesema.

Mkurugenzi huyo amesema, “mashuleni, vituo vya afya tuliweka vifaa kwa kunawa kwa maji safi tiririka, tunawe mikono.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!