Friday , 3 May 2024
Habari za SiasaTangulizi

Ole Sabaya akamatwa

Spread the love

 

ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Lengai ole Sabaya, ametiwa mbaroni jijini Dar es Salaam. Anaripoti Saed Kubenea, Dar es Salaam … (endelea).

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), Kamishena wa Polisi, Salum Hamduni, amethibitisha kukamatwa kwa Sabaya na kuongeza kuwa taasisi yake, inamshikilia mwanasiasa huyo, kwa ajili ya mahojiano.

Anasema, Sabaya anashikiliwa kutokana na kutokana na tuhuma mbalimbali zinazomkabili.

Hata hivyo, Hamduni hakuzungumzia suala hilo kwa undani. Aliishia kusema, “ni kweli kuwa Takukuru inamshikilia Sabaya, kwa mahojiano ya tuhuma mbalimbali za matumizi ya madaraka na rushwa, wakati akiwa mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro.”

Kwa habari zaidi, soma gazeti la Raia Mwema, toleo la leo Ijumaa – Mhariri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!