Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kigogo Bandari aliyetoroka, apandishwa kizimbani kwa utakatishaji fedha
Habari Mchanganyiko

Kigogo Bandari aliyetoroka, apandishwa kizimbani kwa utakatishaji fedha

Pingu
Spread the love

 

ALIYEKUWA Mhasibu katika Bandari ya Kigoma, Madaraka Robert Madaraka, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, kwa tuhuma za utakatishaji fedha na uhujumu uchumi. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), mkoani Kigoma, Stephen Mafipa, Madaraka amepandishwa kizimbani leo tarehe 28 Mei 2021.

Madaraka anadaiwa kuisababisha Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), hasara ya Sh. 619,278,260.

“Takukuru kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, tunamfikisha mahakamani aliyekuwa Mhasibu Bandari ya Kigoma, kwa tuhuma za ufujaji na ubadhirifu, kuisababisha TPA hasara ya Sh. 619,278,260.52 pamoja na utakatishaji fedha,” amesema taarifa ya Mafipa.

Taarifa ya Mafipa imesema kuwa, Madaraka ambaye awali alitoroka, ataunganishwa na washtakiwa wengine wanne, katika Shauri la Uhujumu Uchumi Na. 5/2020, linaloendelea mahakamani hapo.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni, Eliya Stephano Ntinyako, Mkurugenzi wa Kampuni ya Ntinyako Company Limited. Morris Charles Mchindiuza, aliyekuwa Meneja wa Bandari Kigoma. Herman Ndiboto Shimbe, aliyekuwa Afisa Uhasibu TPA Kigoma na Lusubilo Anosisye Mwakyusa, aliyekuwa Afisa Rasilimali watu TPA Kigoma.

“Uchunguzi wa Takukuru Makao Makuu ulibaini kwamba, mtuhumiwa huyu alitoroka kabla ya ofisi yetu kuanza uchunguzi Februari 2020.

“Hivyo basi, tunapenda kuuarifu umma kuwa, ofisi yetu iliendelea kumtafuta mtuhumiwa huyu hadi ilipofanikiwa kumpata na hivi leo atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili,” imesema taarifa ya Mafipa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mafipa, Madaraka anatuhumiwa kuongoza genge la kufanya ubadhirifu wa fedha, katika kituo cha Bandari ya Kigoma, wakati akiwa mhasibu katika kituo hicho.

Mbali na kufikishwa kizimbani, taarifa ya Mafipa imesema Takukuru inaendelea na uchunguzi wa tuhuma nyingine zinazomkabili Madaraka.

“Sambamba na kumuunganisha Madaraka katika shauri hili, uchunguzi wa TAKUKURU Makao Makuu bado unaendelea kufanyika dhidi yake, kwa tuhuma zingine za uhujumu uchumi na kuisababishia hasara TPA,” imesema taarifa ya Mafipa na kuongeza:

“Mara baada ya uchunguzi huo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake pamoja wengine walioshirikiana naye.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!