Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Tuhuma za rushwa: Mwenyekiti CCM akwepa jela, alipa faini
Habari Mchanganyiko

Tuhuma za rushwa: Mwenyekiti CCM akwepa jela, alipa faini

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tawi la Maisaka mkoani Manyara, Bakari Yangu, amekwepa kifungo cha miaka miwili gerezani, kwa kulipa faini ya Sh. 300,000, baada ya kukutwa na hatia katika kesi ya kuomba rushwa, iliyokuwa inamkabili kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Katika kesi hiyo Na. CC.24/2020, Bakari alidaiwa kuomba na kupokea rushwa ya Sh. 200,000, kutoka kwa Mwinjilisti wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mtaa wa Komoto mkoani humo, Daniel Tango, ili amuachie kiwanja kilichokuwa mali ya CCM.

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa tarehe 28 Mei 2021 na Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), mkoani Manyara, Holle Makungu.

Taarifa ya Makungu imesema kuwa, baada ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Simon Kobero, kutoa hukumu hiyo jana tarehe 27 Mei 2021, Bakari alilipa faini hiyo na kukwepa kwenda jela.

“Baada ya kukiri makosa yake, mahakama ilitoa adhabu hiyo, ambapo mshtakiwa Bakari aliweza kulipa Sh. 300,000 na hivyo kukwepa kutumikia kifungo cha miaka miwili jela,” imesema taarifa ya Makungu.

Ikielezea mchakato wa kesi hiyo, taarifa ya Makungu imesema, hukumu hiyo ilitolewa baada ya mshtakiwa huyo kukiri makosa yake.

“Bakari amehukumiwa baada ya kukiri makosa ya kuomba na kupokea rushwa ya Sh. 200,000 kutoka kwa Mwinjilisti Tango, kinyume cha kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya 2007, ili wamwachie mwinjilisti huyo kiwanja ambcho mwenyekiti huyo alidai ni mali ya CCM,” imesema taarifa ya Makungu.

Kesi hiyo Na. CC.24/2020, ilifikishwa mahamani hapo na mawakili wa Takukuru, Martin Makani, akisaidiwa na Evelyne Onditi, tarehe 26 Juni 2020.

Awali, Bakari alikana makosa yake, lakini baada ya Takukuru kuwasilisha mahakamani hapo vilelezo na ushahidi uliomtia hatiani, aliamua kukiri makosa yake.

“Baada ya kukana makosa yake, mawakili waliwasilisha vilelezo na ushahidi ulioiwezesha mhakama kumuona mshtakiwa ana kesi ya kujibu, baada ya kutakiwa kujitetea, aliamua kutoisumbua mahakama kwa kukiri makosa yae yote ya kuomba na kupokea rushwa kama alivyoshtakiwa,” imesema taarifa ya Mkaungu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!