Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba: Ama zetu, Ama zao, mashabiki elfu 10 ruksa
Michezo

Simba: Ama zetu, Ama zao, mashabiki elfu 10 ruksa

Haji Manara, Msemaji wa Simba
Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa marudiano wa Ligi Mabingwa Afrika dhidi ya Kaizer Chiefs, klabu ya Simba imekuja na kauli mbiu ya ‘Ama zetu, Ama zao’ ambayo yenye lengo la kupindua matokeo ili waweze kufuzu kwenye hatua ya nusu fainali. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa robo fainali utachezwa siku ya Jumamosi ya tarehe 22, Mei 2021 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, majira ya saa 10 jioni.

Afisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa timu hiyo itahakikisha inafuzu licha ya kuruhusu mabao 4-0, ugenini na wataingia na slogani ya ‘Ama zetu, Ama zao’.

“Wanasimba wanataka kufuzu, hatutaki kujitahidi, Simba siyo timu ya kujitahidi, ni timu ya kufuzu na mashabiki wanaamini timu yao inaweza na kauli mbiu yetu itakuwa Ama zeta ma zao,” alisema Haji.

Katika hatua nyingine msemaji huyo, amesema kuwa mpaka sasa wameruhusiwa kuingiza mashabiki 10,000 licha ya kufanya juhudi za kutaka kuongezewa.

“Mpaka sasa tumeruhusiwa mashabiki 10,000 lakini tunaendelea kuomba kuongeza, naomba uwanjani rangi iwe nyekundu na nyeupe,” aliongezea Haji.

Ili Simba ifuzu kwenye hatua ya nusu fainali inahitaji kupata ushindi wa bao 5 na kuendelea bila kuruhusu nyavu zao kuruhu bao.

Kikosi hiko kilirejea Jumatatu kutokea Afrika Kusini na siku ya jana Jumanne ya tarehe 18 Mei, 2021 waliingia kambini kwa kuanza maandalizi ya kuwawinda Kaizer Chiefs ambao watawasili muda wowote kuanzia leo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

error: Content is protected !!