Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Michezo Mwamuzi aliyekataa bao la Yanga dhidi ya Namungo afungiwa
Michezo

Mwamuzi aliyekataa bao la Yanga dhidi ya Namungo afungiwa

Spread the love

Mwamuzi msaidizi namba moja Abdulaziz Ally aliyechezesha mchezo wa Namungo Fc dhidi ya Yanga ameondelewa kwenye orodha ya waamuzi kwa michezi mitatu mara baada ya kumudu mchezo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo namba 257, ulichezeshwa Jumamosi ya tarehe 13 Mei, 2021 kwenye Uwanja wa Majaliwa uliopo Ruangwa, Lindi na kumaliza kwa suluhu ya bila kufungana.

Maamuzi hayo yametolewa hii leo na kamati ya uwendeshaji na usimamizi wa Ligi (kamati ya saa 72) kwa kuzingatia kanuni ya 40:1(2.1) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa waamuzi.

Mwamuzi huyo amekumbana na adhabu hiyo mara baada ya kukataa bao la Yacouba Sogne aliyeunganisha kona ya Saido Ntibanzokiza.

Katika hatua nyingine kamati hiyo imeitoza faini kya shilingi 500,000 klabu ya Yanga kwa kosa la kuingia Uwanjani kupitia mlango wa mashabiki badala ya malango maalumu kwenye mchezo dhidi ya Namungo.

Adhabu hiypo pia imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 45(1) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa klabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za UEFA

Spread the love  HATIMAYE leo hii ndio kitaeleweka nani aende Nusu Fainali...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

error: Content is protected !!