Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Mwamuzi aliyekataa bao la Yanga dhidi ya Namungo afungiwa
Michezo

Mwamuzi aliyekataa bao la Yanga dhidi ya Namungo afungiwa

Spread the love

Mwamuzi msaidizi namba moja Abdulaziz Ally aliyechezesha mchezo wa Namungo Fc dhidi ya Yanga ameondelewa kwenye orodha ya waamuzi kwa michezi mitatu mara baada ya kumudu mchezo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo namba 257, ulichezeshwa Jumamosi ya tarehe 13 Mei, 2021 kwenye Uwanja wa Majaliwa uliopo Ruangwa, Lindi na kumaliza kwa suluhu ya bila kufungana.

Maamuzi hayo yametolewa hii leo na kamati ya uwendeshaji na usimamizi wa Ligi (kamati ya saa 72) kwa kuzingatia kanuni ya 40:1(2.1) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa waamuzi.

Mwamuzi huyo amekumbana na adhabu hiyo mara baada ya kukataa bao la Yacouba Sogne aliyeunganisha kona ya Saido Ntibanzokiza.

Katika hatua nyingine kamati hiyo imeitoza faini kya shilingi 500,000 klabu ya Yanga kwa kosa la kuingia Uwanjani kupitia mlango wa mashabiki badala ya malango maalumu kwenye mchezo dhidi ya Namungo.

Adhabu hiypo pia imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 45(1) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa klabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!