Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo PSG hatihati kutetea ubingwa Ufaransa
Michezo

PSG hatihati kutetea ubingwa Ufaransa

Spread the love

 

HUENDA kocha Mauricio Pochettino wa kikosi cha PSG, akawa kwenye wakati mgumu wa kutetea taji lake la Ligu Kuu Ufaransa baada ya kuwa nyuma kwa pointi moja nyuma ya Lille wanaongoza ligi hiyo, huku ukiwa umesalia mchezo mmoja. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Ligi hiyo ambayo itamalizika mwisho wa wiki hii, huku klabu ya Lille huenda ikavunja ufalme wa PSG kwa kutwaa kombe hilo kama ikishinda mchezo wake wa mwisho.

Kwa sasa Lille wanapointi 80 na michezo 37, baada ya kupata suluhu kwenye mchezo wa jana dhidi ya St-Ettienne, wakati PSG wakishika nafasi ya pili wakiwa na pointi 79 na michezo 38, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0, mbele ya Reims.

Mauricio Pochettino, Kocha wa PSG

Kwenye michezo ijayo ya mwisho PSG atakuwa ugenini kumenyana na Brest inayoshika nafasi ya 16, kwenye msimamo, huku Lille wakiwa na matumaini makubwa ya ubingwa nao watakuwa ugenini kukipiga na Angers inayoshika nafasi ya 12 kwenye msimamo.

PSG kwa sasa ndiyo bingwa mtetezi wa taji hilo ambalo amelitwaa mara ya tatu mfululizo na kuweka rekodi ya kulichukua mara saba katika kipindi cha miaka 10.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!