Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari Wazee Dar wamwomba Rais Samia kudumisha utawala bora
HabariHabari Mchanganyiko

Wazee Dar wamwomba Rais Samia kudumisha utawala bora

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

BARAZA la Wazee la Mkoa wa Dar es Salaam, limemuomba Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, aongeze juhudi katika uimarishwaji misingi ya utawala bora. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es salaam..(endelea).

Wito huo umetolewa leo Ijumaa, tarehe 7 Mei 2021 na Salum Matimbwa, Mwenyekiti Baraza la Wazee Mkoa wa Dar es Salaam, katika Mkutano wa Rais Samia na Wazee wa mkoa huo, unaofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City.

“Kuhusu utawala bora, tunakupongeza kwa jinsi ambavyo wewe na serikali yako mnavyosimamia na kutekeleza masulaa mbalimbali ya utawala bora katika nchi yetu, ombi letu tunaomba juhudi hizi ziendelee katika kushughulikia kero za wananchi pamoja na malalamiko yao,” amesema Mzee Matimbwa.

Salum Matimbwa, Mwenyekiti wa Wazee Mkoa wa Dar es Salaam

Wakati huo huo, Mzee Matimbwa ameiomba Serikali ya Rais Samia, iwashirikishe wananchi katika masuala mbalimbali ikiwemo kwenye utafutaji suluhu za changamoto zao.

“Sambamba na hilo, tunaomba vyombo vya ulinzi na usalama kufanya kazi kwa kufuata sheria, kanuni na miongozi na pale inapobidi wananchi washirikishwe ipasavyo kuondoa matatizo madogo madogo. Hili kama mnavyo lisimamia vizuri likiendelezwa ustawi wa utawala bora na usalama utaendelea katika nchi yetu,” amesema Mzee Matimbwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!