Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar yawakamata 161 tuhuma wizi magari, pikipiki
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar yawakamata 161 tuhuma wizi magari, pikipiki

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Dar es Salaam
Spread the love

 

JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, nchini Tanzania, limewakamata watu 161 kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo za wizi wa magari, vifaa vya magari na pikipiki. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Alhamisi, tarehe 6 Mei 2021 na Kanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na waandishi wa habari, jijini humo.

Amesema, tarehe 26 Aprili hadi 2 Mei 2021, Polisi kanda hiyo, liliendelea na oparesheni maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam na kukamata watuhumiwa 161.

“Katika idadi ya watuhumiwa hao 161, watuhumiwa watano vinara wa wizi wa pikipiki, wamekamatiwa Zanzibar wakiwa na pikipiki 40 za wizi.”

“Watuhumiwa hawa wamekuwa wakiiba pikipiki hapa jijini Dar es Salaam, Morogoro na Pwani na kuzipeleka Zanzibar kutafuta wateja,” amesema Mambosasa.

Amesema, watuhumiwa hao wataletwa Dar es Salaam kutoka Zanzibar pamoja na vielelezo na watafikishwa mahakamani baada ya kukamilisha taratibu zote za kisheria.

Aidha, katika oparesheni hiyo, Kamanda Mambosasa amesema, “tulifanikiwa kukamata magari mawili aina ya Toyota Noah lenye namba T 770 ACY na Toyota IST yenye namba T 137 DMM magari haya yote yaliibiwa Aprili na kupatikana Mei 2021.”

Amesema, vilevile walikamata silaha ndogo bastola aina ya BROWNING COURT yenye namba B113558 TZ CAR 110526 ambayo iliibiwa tarehe 7 Aprili 2021, maeneo Chanika Lubakaya nyumbani kwa mtoa taarifa, ambapo kikosi kazi cha Jeshi la Polisi kilifanya ufuatiliaji na kufanikiwa kuikamata silaha hiyo tarehe 01 Mei 2021, maeneo hayohayo ya chanika.

Kamanda huyo wa polisi amesema, katika oparesheni hiyo, walifanikiwa kukamata vitu mbalimbali vidhaniwavyo kuwa ni vya wizi kama kama vile; pikipiki 91, TV za aina mbalimbali, ving’amuzi vyake, Subwoofer na Computer .

Pia, walikamata, pikipiki za matairi matatu (Bajaji) nne, Bello 24 za nguo za mitumba, vifaa vya umeme, simu za mkononi, mitungi ya gesi na vipuri vya magari kama vile milango ya magari, taa za magari, mabampa ya magari, Power window na Gia box.

“Oparesheni hii ni endelevu, itaendelea kufanyika ili kuhakikisha jiji letu linaendelea kuwa shwari,” amesema Mambosasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Je, miji ya Uingereza inafilisika?

Spread the loveMNAMO 1890, mwandishi mmoja wa habari Mmarekani aitwaye Julian Ralph...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

error: Content is protected !!