Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mzee miaka 61 akutwa na funguo 83 bandia, misumari 47 Dar
Habari Mchanganyiko

Mzee miaka 61 akutwa na funguo 83 bandia, misumari 47 Dar

Dk. Lazaro Mambosasa
Spread the love

 

KAMANDA wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema, wanamshikilia Mzee Said Abdallah (61), baada ya kumkuta akiwa na funguo bandia 83, misumari ya aina mbalimbali 47 anazodaiwa kutumia kwa wizi. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari, leo Alhamisi, tarehe 6 Mei 2021, Mambosasa amesema, Mzee huyo, anatuhumiwa kwa wizi kwenye Maghala na maduka kwa kutumia funguo bandia.

Amesema, Mzee huyo Mkazi wa Mbagala Kilungule, alikamatwa tarehe 04 Mei 2021, huko Mbagala Kilungule akiwa na funguo bandia 83, misumari ya aina mbalimbali 47 ambayo ni malighafi za kutengenezea funguo bandia.

“Mtuhumiwa alihojiwa na kukiri kufanya uhalifu tangu mwaka 2013 maeneo mbalimbali ya Jiji kwa kutumia funguo bandia,” amesema Mambosasa

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!