Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Michezo Baada ya kuiadhibu Real Madrid, Tuchel awamwagia sifa wachezaji wake
Michezo

Baada ya kuiadhibu Real Madrid, Tuchel awamwagia sifa wachezaji wake

Spread the love

 

BAADA ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Real Madrid, kocha wa kikosi cha Chelsea, Thomas Tuchel ametoa pongezi kwa wachezaji wake kwa kufanikisha timu hiyo kufuzu kwenye fainali ya Ligi ya  Mabingwa Ulaya kwa kuwa ulikuwa mchezo mgumu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa nusu fainali ulichezwa jana kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, ambapo Chelsea ilifanikiwa kuungana na Manchester City kwenye mchezo wa fainali utakaopigwa jijini Instabul nchini Uturuki tarehe 28 Mei, 2021.

Baada ya mchezo huo kumalizika kocha wa Chelsea, Tuchel alisema walistahili kushinda licha ya kuwa mchezo mgumu kwa kuwa Madrid, walimiliki mpira kwa asilimia kubwa ila wao walikuwa bora kwenye mashambulizi ya kushtukiza (counter attack).

“Ulikuwa mchezo mgumu kwa sababu Real Madrid, walikuwa na umiliki mzuri wa mpira na walitufanya sisi kuangaika zaidi, lakini baadae tulikuwa hatari sana kwenye mashulizi ya kushtukiza na hatukupoteza hali yetu ya kuzuia,” alisema Tuchel na kuongeza;

“Kipindi cha pili tulikuwa bora sana, kwa mfumo wa kuzuia na tungeweza kupata bao la mapema sana na tungeweza kufunga zaidi, ni mafanikio makubwa na hongera kwa timu.”

Mabao ya jana ya Chelsea yalifungwa na Timo Werner kwenye dakika ya 28, na bao la pili likiwekwa kambani na Mason Mount kwenye dakika ya 85.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

error: Content is protected !!