Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia amlilia Teddy Mapunda
Habari Mchanganyiko

Rais Samia amlilia Teddy Mapunda

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema, ameomboleza kifo cha Teddy Mapunda, akisema nchi imepoteza mwanamke hodari na mchaka kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam ... (endelea). 

Samia ametoa salamu hizo kupitia kurasa zake za kijamii, kufuatia kifo cha Teddy kilichotokea Jumanne ya tarehe 4 Mei 2021, katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam.

Ni baada ya kuugua kwa muda mfupi, alipokuwa akishiriki chakula cha jioni na marafiki zake, katika Hotel ya Serena, jijini humo.

Rais Samia ameandika “Nimehuzunishwa na kifo cha Teddy Mapunda. Tumepoteza Mwanamke hodari, mchapakazi, mbunifu, mahiri na aliyedhibitisha kwa vitendo kuwa Wanawake wanaweza.”

“Nitamkumbuka kwa jinsi alivyojitoa kwa Chama na Serikali na alivyoipenda nchi yake. Mungu amweke mahali pema peponi, Amina.”

Enzi za uhai wake, Teddy alikuwa mwanamichezo na alikuwa mjumbe kwenye kamati ya hamasa ya Taifa Star.

Pia, alikuwa Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Habari Tanzania (MCL), akiwa kama makamu mwenyekiti wa kamati ya fedha na utawala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa aanika mafanikio ya TMA

Spread the loveSHUGHULI za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), zimeimarika...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!