Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Rais Samia amlilia Teddy Mapunda
Habari Mchanganyiko

Rais Samia amlilia Teddy Mapunda

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema, ameomboleza kifo cha Teddy Mapunda, akisema nchi imepoteza mwanamke hodari na mchaka kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam ... (endelea). 

Samia ametoa salamu hizo kupitia kurasa zake za kijamii, kufuatia kifo cha Teddy kilichotokea Jumanne ya tarehe 4 Mei 2021, katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam.

Ni baada ya kuugua kwa muda mfupi, alipokuwa akishiriki chakula cha jioni na marafiki zake, katika Hotel ya Serena, jijini humo.

Rais Samia ameandika “Nimehuzunishwa na kifo cha Teddy Mapunda. Tumepoteza Mwanamke hodari, mchapakazi, mbunifu, mahiri na aliyedhibitisha kwa vitendo kuwa Wanawake wanaweza.”

“Nitamkumbuka kwa jinsi alivyojitoa kwa Chama na Serikali na alivyoipenda nchi yake. Mungu amweke mahali pema peponi, Amina.”

Enzi za uhai wake, Teddy alikuwa mwanamichezo na alikuwa mjumbe kwenye kamati ya hamasa ya Taifa Star.

Pia, alikuwa Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Habari Tanzania (MCL), akiwa kama makamu mwenyekiti wa kamati ya fedha na utawala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!