Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia ateta na Rais mstaafu Obasanjo Ikulu Dodoma
Habari za SiasaTangulizi

Samia ateta na Rais mstaafu Obasanjo Ikulu Dodoma

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Nigeria, Olusegun Obasanjo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mazungumzo hayo, yamefanyika leo Jumatatu, tarehe 3 Mei 2021, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma.

Obasanjo ametoa salamu zake za rambirambi kwa Rais Samia, kufuatia vifo vya waliokuwa marais wa wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa na Hayati John Pombe Magufuli.

Hayati Mkapa, alifariki dunia tarehe 23 Julai, 2020 na Hayati Magufuli, aliaga dunia tarehe 17 Machi, 2021.

Rais huyo mstaafu, amempongeza, Rais Samia kwa kupokea kijiti cha kuwa Rais wa Tanzania na amemtakia heri katika majukumu yake.

Aidha, katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamezungumzia hali ya usalama Barani Afrika na umuhimu wa wakuu wa nchi kujadiliana na kutafuta suluhisho la migogoro hiyo ambayo inasababisha vifo vya watu wasio na hatia hasa wanawake na watoto.

Pia, viongozi hao, wamezungumzia masuala ya maendeleo hasa katika uchumi na kusisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kuongeza ushirikiano na kuondoa vikwazo vya biashara na uwekezaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!