Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Katibu mkuu CCM amuomba Rais Samia aongeze mishahara
Habari za Siasa

Katibu mkuu CCM amuomba Rais Samia aongeze mishahara

Katibu Mkuu mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo
Spread the love

 

KATIBU Mkuu mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, aboreshe maslahi ya watumishi wa umma, kama Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho 2020-2025, inavyoelekeza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Chongolo ametoa wito huo leo Jumamosi tarehe 1 Mei 2021, katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazo duniani ‘Mei Mosi’, iliyofanyika jijini Mwanza, ambapo Rais Samia ni mgeni rasmi .

Chongolo aliyeteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho jana Ijumaa, ametoa wito huo baada ya wafanyakazi walioshiriki maadhimisho hayo, kubeba mabango yenye ujumbe wa kudai ongezeko la mishahara.

Mabango hayo yalibeba kauli mbiu iliyosomeka “Maslahi bora, mishahara juu, kazi iendelee’.

“Leo mimi ni mara ya kwanza kusimama mbele ya halaiki hii, lakini si mgeni wa kazi za kusimama mbele ya watu, niseme sikukuu hii kwetu ni sehemu ya wajibu wa msingi sana kuzishiriki lakini pia kuhakikisha tunazifanya zijenge tabasamu kwa wafanyakazi,” amesema Chongolo

“Mimi sitasema mengi, nihitimishe kwa kusema, nina ujumbe wa kwaya moja ya Makongoro wanasema wanasubiri mama useme neno ili mioyo yao ipone. Nami sina shaka kwani ilani imeahidi masilahi bora ya watumishi, sina shaka kwa hilo ule ujumbe wa TUCTA (Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania), mliofikisha kwa kwaya utafika,” amesema huku akishangiliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!