Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafanyakazi Dodoma yaomba nyongeza ya mishahara
Habari Mchanganyiko

Wafanyakazi Dodoma yaomba nyongeza ya mishahara

Spread the love

 

VYAMA vya wafanyakazi Mkoa wa Dodoma, wameiomba Serikali kuona uwezekano wa kuongeza mishahara kama inavyotakiwa kisheria. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Wametoa ombi hilo, leo Jumamosi, tarehe 1 Mei 2021, wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei Mosi yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Mei Mosi 2021 ni; Maslahi bora, mishahara juu, kazi iendelee.

Lizz Msechu, mwenyekiti Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Mkoa wa Dodoma amesema, kitendo cha wafanyakazi kutopandishiwa mishahara yao kwa kipindi cha miaka zaidi ya mitano, kinawafanya wafanyakazi kuishi maisha mabaya.

“Tunaomba serikali ione umuhimu wa kurejesha utaratibu wa kuongeza nyongeza za mishahara ili kuwe za kuwafanya wafanyakazi kuweza kuishi maisha ambayo yatakuwa na unafuu”amesema Msechu.

Pia, amesema wafanyakazi wanaiomba serikali kuona namna ya kubadili ulipaji wa kodi kwani watumishi wanajikuta wakilipa kodi mara mbili kwa maana ya kulipa kodi moja kwa moja inayokatwa kwenye mshahara na kulipa kodi wanapokwenda kununua bidhaa.

Katika hatua nyingine, amesema baadhi ya waajiri wamekuwa hawataki kuanzishwa kwa mabaraza ya kazi jambo ambalo linakinzana na utaratibu.

Akizungumzia kuhusu mafao ya wastaafu, Msechu amesema ni changamoto kubwa kwa kuwacheleweshea mafao yao wastaafu mafao tao.

Dk. Binirithi Mahenge, mkuu wa Mkoa wa Dodoma akijibu maombi hayo ya wafanyakazi amewaagiza waajiri wote kuhakikisha wanaanzisha mabaraza ya wafanyakazi katika sehemu za kazi.

Mbali na hilo, ameziagiza taasisi zote zinazotoa mafao ya wastaafu kuhamikisha wanatoa mafao kwa wakati badala ya kuwacheleweshea mafao yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!