Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Vijana kupatiwa mbinu tete, stadi za maisha
Habari Mchanganyiko

Vijana kupatiwa mbinu tete, stadi za maisha

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga
Spread the love

 

NUSRAT Hanje, Mbunge wa Viti Maalum asiye na chama bungeni, ameihoji serikali ni kwanini haioni umuhimu wa kurekebisha mfumo wa elimu na kuingiza mbinu tete za stadi za maisha ili kuwajengea uwezo wa kiushindani vijana wanaohitimu. Anaripoti Nasra Bakari na Jemima Samweli, DMC … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Ijumaa, tarehe 30 April 2021, bungeni jijini Dodoma, katika kipindi cha maswali na majibu.

“Je, ni kwanini serikali, haioni umuhimu wa kurekebisha mfumo wa elimu na kuingiza mbinu tete za stadi za maisha ili kuwajengea uwezo wa kiushindani vijana wanaohitimu na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira,” alihoji Hanje

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga alisema, Serikali inatambua umuhimu wa kuwawezesha wanafunzi kupata stadi za maisha na mbinu tete ili kuwa na uwezo wa kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo swala la ajira.

Alisema, Serikali imekuwa ikiboresha mitaala kila kunapokuwa na hitaji la kisayansi, kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na kiteknolojia.

“Katika kipindi cha mwaka 2021/2022, Serikali itafanya mapitio ya mitaala ya shule za msingi na sekondari ili kuingiza stadi mbalimbali kama vile stadi za maisha hususani stadi za karne ya 21 na mbinu tete,” alisema Kipanga na kuongeza:

“Stadi za Karne ya 21 ni pamoja na tunduizi, ubunifu, ushirikiano, uongozi na stadi za teknolojia ya habari na mawasiliano stadi na mbinu hizi zitasaidia kuwajengea vijana uwezo wa kiushindani katika soko la ajira.” Alisema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!