Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari Chongolo amrithi Dk. Bashiru CCM, Shaka…
HabariHabari za Siasa

Chongolo amrithi Dk. Bashiru CCM, Shaka…

Daniel Chongolo katibu mkuu wa Ccm
Spread the love

 

DANIEL Chongolo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, mkoani Dar es Salaam, amethibitishwa na Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Chongolo, amethibitishwa leo Ijumaa, tarehe 30 Aprili 2021, baada ya jina lake, kuwasilishwa na Mwenyekiti mpya wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan.

Katibu wa Itikadi na uenezi CCM, Shaka Hamidu Shaka

Chongolo ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari, anachukua nafasi ya Dk. Bashiru Ally, aliyeiacha tarehe 26 Februari 2021, baada ya kuteuliwa na Hayati Rais John Magufuli, kuwa katibu mkuu kiongozi.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Dk. Bashiru Ally

Pia, kikao hicho cha Halmashauri Kuu, kimemteua, Shaka Hamidu Shaka, kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi.

Shaka aliyewahi kuwa kaimu katibu mkuu wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), anachukua nafasi ya Humphrey Polepole, ambaye kwa sasa ni mbunge wa kuteuliwa.

Shaka, alikuwa katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro, alisimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma za rushwa za kumpata Meya wa Manispaa ya Morogoro.

Tuhuma hizo, zilitolewa hadharani na Hayati Magufuli, tarehe 11 Februari 2021, wakati anazindua Soko Kuu la Mkoa wa Morogoro.

Pia, Halmashauri Kuu hiyo chini ya mwenyekiti wake, Rais Samia, imemteua Christina Mdeme, kuwa naibu katibu mkuu wa CCM- Bara, akichukua nafasi ya Rodrick Mpogolo.

1 Comment

  • Kwa hiyo shutuma za JPM dhidi ya Shaka zilikuwa ni uzushi? Ripoti iko wapi? Alichunguzwa na Takukuru?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!