Saturday , 27 April 2024
Habari za Siasa

Bunge latengua kanuni

Bunge la Tanzania
Spread the love

 

BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limetengua kanuni kanuni ya 160 (1) ili kuruhusu wasio wabunge kuingia ukumbini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kanuni hiyo imetenguliwa leo Alhamisi tarehe 22 Aprili 2021, baada ya Jenista Muhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu kutoa hoja ya utenguzi wa kanuni hiyo.

Hoja hiyo imeungwa mkono na wabunge baada ya kuhojiwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai kutokana na ujio wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuhutubia Bunge kwa mara ya kwanza.

Utenguzi wa kanuni hiyo, sasa unaruhusu mtu asiyekuwa mbunge kuingia katika ukumbi wa bunge, Rais Samia pamoja na viongozi wengine wa ngazi za juu nchini, wataingia ndani ya ukumbi huo.

Mbali na Rais Samia, viongozi wengine watakaoingia ndani ya ukumbi wa bunge ni pamoja na Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi; Makamu wa Rais Tanzania, Dk. Philip Mpango; Makamu wa Kwanza na wa Pili wa Rais Zanzibar; Jaji Mkuu wa Tanzania; Jaji Mkuu wa Zanzibar; Spika wa Bunge la Afrika Mashariki na Spika wa Baraza la Wawakilishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!