Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge wapigwa ‘stop’ kuvaa tai nyekundu
Habari za Siasa

Wabunge wapigwa ‘stop’ kuvaa tai nyekundu

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania
Spread the love

 

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amewataka wabunge kutovaa tai nyekundu, bungeni jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ni leo Alhamisi saa 10:00 jioni, tarehe 22 Aprili 2021, wakati Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, atakapokwenda kulihutubia Bunge hilo.

Rais Samia, anakwenda kuhutubia Bunge kwa mara ya kwanza, tangu alipoingia madarakani tarehe 19 Machi 2021, akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Hayati John Pombe Magufuli, aliyefariki 17 Machi 2021 na mwili wake, kuzikwa Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Saluhu akihutubia Taifa mara baada ya kuapishwa

Akitoa tangazo hilo leo asubuhi, Spika Ndugai amesema, kukiwa na kiongozi mkubwa wa nchi anapokwenda kuhutubia Bunge, tai nyekundu inayoonyesha mamlaka inavaliwa na mtu mmoja pekee

“Tai nyekundi ni ya mamlaka, inapaswa kuvaliwa na mtu mmoja tu. Jioni msije mmevaa tai nyekundi, mtarudia getini,” amesema Spika Ndugai huku wabunge wakishangilia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!