Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM aomba hospitali, serikali yamjibu
Habari za Siasa

Mbunge CCM aomba hospitali, serikali yamjibu

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

JAFARI Chege, Mbunge wa Rorya (CCM), mkoani Mara, amehoji serikali lini itakipandisha hadhi kituo cha afya Kinesi kinachohudumia vijiji 27 ili kiwe hospitali. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Chege amehoji suala hilo, leo Alhamisi, tarehe 28 April 2021, Bungeni jijini Dodoma, wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

“Je, ni lini Kituo cha Afya Kinesi kitapandishwa hadhi na kuwa Hospitali kamili
kutokana na Kituo hicho kuhudumia wananchi zaidi ya Vijiji 27 katika Jimbo la Rorya,” amehoji Chege

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Tamisemi-David Silinde amesema, ili kuboresha huduma za afya katika wilaya ya Rorya Sh.1.5 bilioni zimetolewa kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa hospitali ya halmashauri.

Amesema, katika mwaka wa fedha 2020/21, Serikali imetenga Sh.500 milioni kwa ajili ya ujenzi wa wodi tatu na Sh.500 milioni, imetolewa kwa ajili ya vifaa vya tiba.

Silinde amesema, “Serikali haitakipandisha hadhi kituo cha afya Kinesi kwa kuwa, bado kinaendelea na ujenzi huo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!