Thursday , 28 March 2024
Habari za Siasa

Bunge latengua kanuni

Bunge la Tanzania
Spread the love

 

BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limetengua kanuni kanuni ya 160 (1) ili kuruhusu wasio wabunge kuingia ukumbini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kanuni hiyo imetenguliwa leo Alhamisi tarehe 22 Aprili 2021, baada ya Jenista Muhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu kutoa hoja ya utenguzi wa kanuni hiyo.

Hoja hiyo imeungwa mkono na wabunge baada ya kuhojiwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai kutokana na ujio wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuhutubia Bunge kwa mara ya kwanza.

Utenguzi wa kanuni hiyo, sasa unaruhusu mtu asiyekuwa mbunge kuingia katika ukumbi wa bunge, Rais Samia pamoja na viongozi wengine wa ngazi za juu nchini, wataingia ndani ya ukumbi huo.

Mbali na Rais Samia, viongozi wengine watakaoingia ndani ya ukumbi wa bunge ni pamoja na Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi; Makamu wa Rais Tanzania, Dk. Philip Mpango; Makamu wa Kwanza na wa Pili wa Rais Zanzibar; Jaji Mkuu wa Tanzania; Jaji Mkuu wa Zanzibar; Spika wa Bunge la Afrika Mashariki na Spika wa Baraza la Wawakilishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

error: Content is protected !!