Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Hoseah ashinda urais TLS
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Hoseah ashinda urais TLS

Spread the love

 

DAKTARI Edward Hoseah, ameibuka mshindi wa urais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS). Anaripoti Regina Mkonde, Arusha … (endelea).

Uchaguzi huo, umefanyika leo Ijumaa tarehe 16 Aprili 2021, katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa Arusha (AICC).

Dk. Hoseah, aliyewahi kuwa mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) kati ya 2006-2015, amewashinda wenzake wanne, katika kinyang’anyiro hicho.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi TLS, Wakili Charles Rwechungura, amesema Dk. Hoseah ameshinda kwa kura 293, kati ya  kura 802 zilizopigwa na mawakili waliojitokeza.

Amesemq, Flaviana Charles amepata kura 223, huku aliyeshika nafasi ya tatu kwenye uchaguzi huo, Shehzada Walli akipata kura 192.

Rwechungura amesema, nafasi ya nne ni Albert Msando aliyepata kura 69 na wa mwisho Francis Stolla alipata kura 17.

Dk. Hoseah ataiongozo TLS kwa kipindi cha mwaka mmoja, kwa mujibu wa katiba ya chama hicho na baada ya kumalizika, akipenda kugombea tena, anaweza kufanya hivyo.

Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Rugemeleza Nshalla, ambaye amemaliza muda wake wa uongozi.

Baadhi ya marais waiowahi kuongoza TLs ni: Charles Rwechungura, Francis Stolla, Tundu Lissu, Fatma Karume na Dk. Rugemeleza Nshalla

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!