Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mgogoro wakulima, wafugani Ruaha kufika tamati
Habari za Siasa

Mgogoro wakulima, wafugani Ruaha kufika tamati

Dk. Damas Ndumbalo
Spread the love

 

UTATUZI wa mgogoro wa muda mrefu kati ya wakulima na wafugaji wanaozunguka Hifadhi ya Taifa Ruaha, upo mbioni kuanza. Anaripoti Mwandiahi Wetu, Dodoma … (endelea).

Waziri wa Maliasil na Utalii Dk. Damas Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo tarehe 16 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma akijibu swali la Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Mbarali.

Mtega alitaka kujua mkakati wa serikali kumaliza migogoro kati ya wakulima na wafugaji wanaozunguka hifadhi hiyo.

“Serikali iliunda kamati iliyojumuisha mawaziri kutoka wizara nane kwa ajili ya kufuatilia na kutatua migogoro ya ardhi nchini. Migogoro iliyofanyiwa kazi na kamati husika ni pamoja na migogoro kati ya wakulima na wafugaji wanaozunguka Hifadhi ya Taifa Ruaha.

“Kamati hiyo imeshafanya tathmini ya migogoro hiyo na kutoa mapendekezo ambayo yameshatolewa maamuzi na Baraza la Mawaziri kwa ajili ya utekelezaji utakaoanza hivi karibuni,” amesema.

Waziri Ndumbaro ameomna wabunge ambao maeneo yao yana changamoto ya migogoro, kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!