Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mgogoro wakulima, wafugani Ruaha kufika tamati
Habari za Siasa

Mgogoro wakulima, wafugani Ruaha kufika tamati

Dk. Damas Ndumbalo
Spread the love

 

UTATUZI wa mgogoro wa muda mrefu kati ya wakulima na wafugaji wanaozunguka Hifadhi ya Taifa Ruaha, upo mbioni kuanza. Anaripoti Mwandiahi Wetu, Dodoma … (endelea).

Waziri wa Maliasil na Utalii Dk. Damas Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo tarehe 16 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma akijibu swali la Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Mbarali.

Mtega alitaka kujua mkakati wa serikali kumaliza migogoro kati ya wakulima na wafugaji wanaozunguka hifadhi hiyo.

“Serikali iliunda kamati iliyojumuisha mawaziri kutoka wizara nane kwa ajili ya kufuatilia na kutatua migogoro ya ardhi nchini. Migogoro iliyofanyiwa kazi na kamati husika ni pamoja na migogoro kati ya wakulima na wafugaji wanaozunguka Hifadhi ya Taifa Ruaha.

“Kamati hiyo imeshafanya tathmini ya migogoro hiyo na kutoa mapendekezo ambayo yameshatolewa maamuzi na Baraza la Mawaziri kwa ajili ya utekelezaji utakaoanza hivi karibuni,” amesema.

Waziri Ndumbaro ameomna wabunge ambao maeneo yao yana changamoto ya migogoro, kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!