Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM, wastaafu watakiwa kutubu
Habari za Siasa

CCM, wastaafu watakiwa kutubu

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  kimewataka viongozi wastaafu na walioko madarakani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na wa serikali, kuwaomba radhi Watanzania. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam… (endelea).

Ni kutokana na dosari zilizojitokeza kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020 ili kuleta utengamano wa Taifa.

Wito huo umetolewa leo tarehe 11 Aprili 2021, mkoani Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, wakati akilihutubia Taifa.

Mwanasiasa huyo amedai kuwa, viongozi hao wanapswa kuomba radhi kwa kosa la kufumbia macho dosari hizo.

“CCM huwa kinawaza nini na kuzungumza nini katika vikao vyake?  Nimetafakari sana je viongozi wake wastaafu waliweza vipi kushiriki huku watu wakilalamika. Kuna sehemu hawa nao wamelibaka sana Taifa letu hawastahili kubeba dhamana ya maisha.

“Angalau Taifa lingeombwa  msahama na viongozi wastaafu wa CCM, ambao waliweza kufurahi na  kushangilia ubunge na udiwani ambao haukuwa haki yao, huku wakijua katika hatua za awali hawakushinda uchaguzi. Hata kama ni kuleta utengamano wa Taifa, tunahitaji apology (kuomba radhi) kwa nchi na Watanzaia,” amesema Mbowe.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!