Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM, wastaafu watakiwa kutubu
Habari za Siasa

CCM, wastaafu watakiwa kutubu

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  kimewataka viongozi wastaafu na walioko madarakani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na wa serikali, kuwaomba radhi Watanzania. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam… (endelea).

Ni kutokana na dosari zilizojitokeza kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020 ili kuleta utengamano wa Taifa.

Wito huo umetolewa leo tarehe 11 Aprili 2021, mkoani Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, wakati akilihutubia Taifa.

Mwanasiasa huyo amedai kuwa, viongozi hao wanapswa kuomba radhi kwa kosa la kufumbia macho dosari hizo.

“CCM huwa kinawaza nini na kuzungumza nini katika vikao vyake?  Nimetafakari sana je viongozi wake wastaafu waliweza vipi kushiriki huku watu wakilalamika. Kuna sehemu hawa nao wamelibaka sana Taifa letu hawastahili kubeba dhamana ya maisha.

“Angalau Taifa lingeombwa  msahama na viongozi wastaafu wa CCM, ambao waliweza kufurahi na  kushangilia ubunge na udiwani ambao haukuwa haki yao, huku wakijua katika hatua za awali hawakushinda uchaguzi. Hata kama ni kuleta utengamano wa Taifa, tunahitaji apology (kuomba radhi) kwa nchi na Watanzaia,” amesema Mbowe.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!