Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Mabadiliko Yanga yanoga, kuitisha Mkutano Mkuu
Michezo

Mabadiliko Yanga yanoga, kuitisha Mkutano Mkuu

Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya Yanga upo mbioni kuitisha mkutano mkuu wa wanachama hivi karibuni huku moja ya ajenda ikiwa ni mabadiliko ya katiba kuelekea mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endela).

Rasimu hiyo ya mabadiliko ilikabidhiwa Desemba 2020, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Mabadiliko ya Uendeshaji wa Klabu ya Yanga, Wakili Alex Mgongolwa na kukabidhiwa Dk. Mshindo Msolwa ambaye ni Mwenyekiti wa Yanga.

Mara baada ya kukabidhiwa Rasimu hiyo, Msolla alisema kinachofuata kwa sasa ni kukutana na viongozi wa matawi na kuwapa elimu juu ya mfumo huo wa mabadiliko na baadaye kuitisha mkutano wa wanachama kwa ajili ya mabadiliko ya katiba.

Taarifa iliyotolea leo na klabu ya Yanga, imeeleza kuwa uongozi huo unajipanga kuitisha mkutano wa wanachama hivi karibuni na kuwataka wanachama kulipia kadi zao kwa njia mbalimbali ili waweze kupata uhalali wa kuingia kwenye mkutano.

Yanga itakuwa klabu ya pili kuingia kwenye mfumo huo wa kisasa wa uendeshaji wa klabu kwa kukaribisha uwekezaji kupitia manunuzi ya hisa kama ilivyokuwa kwa wenzao Simba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!