Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari CAG: Taasisi 10 zimepata hati mbaya, 81 zenye shaka
HabariTangulizi

CAG: Taasisi 10 zimepata hati mbaya, 81 zenye shaka

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)
Spread the love

 

RIPOTI za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa mwaka 2019/20, zimewasilishwa bungeni jijini Dodoma huku taasisi kumi zikipata hata mbaya na 81 zenye shaka. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Ripoti hizo, zimewasilishwa leo Alhamisi tarehe 8 Aprili 2021, na CAG Charles Kichere.

Kichere amewasilishwa jumla ya ripoti 21 zinazojumuisha masuala mbalimbali yaliyojitokeza katika ukaguzi alioufanya kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2020 kwa taasisi nilizozikagua.

CAG huyu amesema, “kwa mwaka huu, nimetoa hati mbaya kwa kumi” huku taasisi 82 zikipata hati zenye shaka.

Amezitaja taasisi hizo kumi kuwa ni; Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Halmashauri ya Wilaya ya Igunga na Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge.

Zingine ni; Halmashauri ya Wilaya ya Urambo, Halmashauri ya Wilaya ya Momba, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Tume ya UNESCO na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Morogoro.

Taasisi 81 zilizopata hati zenye shaka hizi hapa chini, zikiwemo vyama vya siasa, vyuo vikuu, halmashauri na wakala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

error: Content is protected !!