Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Mabadiliko Yanga yanoga, kuitisha Mkutano Mkuu
Michezo

Mabadiliko Yanga yanoga, kuitisha Mkutano Mkuu

Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya Yanga upo mbioni kuitisha mkutano mkuu wa wanachama hivi karibuni huku moja ya ajenda ikiwa ni mabadiliko ya katiba kuelekea mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endela).

Rasimu hiyo ya mabadiliko ilikabidhiwa Desemba 2020, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Mabadiliko ya Uendeshaji wa Klabu ya Yanga, Wakili Alex Mgongolwa na kukabidhiwa Dk. Mshindo Msolwa ambaye ni Mwenyekiti wa Yanga.

Mara baada ya kukabidhiwa Rasimu hiyo, Msolla alisema kinachofuata kwa sasa ni kukutana na viongozi wa matawi na kuwapa elimu juu ya mfumo huo wa mabadiliko na baadaye kuitisha mkutano wa wanachama kwa ajili ya mabadiliko ya katiba.

Taarifa iliyotolea leo na klabu ya Yanga, imeeleza kuwa uongozi huo unajipanga kuitisha mkutano wa wanachama hivi karibuni na kuwataka wanachama kulipia kadi zao kwa njia mbalimbali ili waweze kupata uhalali wa kuingia kwenye mkutano.

Yanga itakuwa klabu ya pili kuingia kwenye mfumo huo wa kisasa wa uendeshaji wa klabu kwa kukaribisha uwekezaji kupitia manunuzi ya hisa kama ilivyokuwa kwa wenzao Simba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!