Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Spika Ndugai awashukia wanaofurahia kifo cha Magufuli
Habari MchanganyikoTangulizi

Spika Ndugai awashukia wanaofurahia kifo cha Magufuli

Spread the love

 

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, amewashukia watu wanaofurahia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Magufuli (61), kilichotokea Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dodoma … (endelea).

Kiongozi huyo wa mhimili wa bunge, amewashukia watu hao leo Jumatatu tarehe 22 Machi 2021, wakati mwili wa Hayati Rais Magufuli ukiagwa na wabunge kwenye viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Hayati Magufuli amefariki dunia katika Hospitali ya Mzena, mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo.

Akizungumzia kifo hicho, Spika Ndugai amewafananisha watu hao na nyani waliofurahia kifo cha mwenye shamba la mahindi, ambaye alikuwa anawazuia kula mahindi yake.

“Sasa iko hadithi ya wale nyani walioshambulia shamba la mkulima kwenye mahindi, wakifurahi sana mahindi yanapokuwa yanaiva wanavuna wanakula, walipopata habari mwenye shamba amefariki wale nyani walifurahi sana.”

“Naamini katika nchi yetu manyani wa namna hii hawakosekani, lakini wakasahau mwaka uliofika wakati mahindi kuiva wakarudi shambani kula mahindi wakasahau mwenye shamba alifariki mwaka jana wakawa wanasikitika,” amesimulia Spika Ndugai.

Spika Ndugai ameshauri Watanzania, wasiwe kama ngedere hao kwa kutofanya mambo mabaya ambayo hayati Rais Magufuli aliyakataza.

“Naamini mwenye shamba amefariki lakini sisi hatutakuwa wale ngedere kusema tutafanya tunavyotaka,” amesema Spika Ndugai.

Kuali hiyo, anaitoa wakati tayari Jeshi la Polisi nchini Tanzania katika maeneo mbalimbali nchini, linawashikilia watu kadhaa kutokana na tuhuma za kufurahia kifo hicho.

Kufuatia maombolezo ya kifo cha Hayati Rais Magufuli, Spika Ndugai amesema wametenga tarehe 30 Machi 2021, kuwa siku maalumu ya kuweka azimio la kumuenzi kiongozi huyo.

 

“Tumetenga tarehe 30 siku tutakayoanza bunge hapa, tutakuwa na programu maalumu ambayo tutaifanya ndani ya ukumbi wa bunge ambapo kutakuwa na azimio maalumu,” amesema Spika Ndugai.

Mwili wa Hayati Rais Magufuli unatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Chato mkoani Geita, Ijumaa tarehe 26 Machi 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!