Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Tanzania wamkamata Askofu Mwamakula
Habari Mchanganyiko

Polisi Tanzania wamkamata Askofu Mwamakula

Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam nchini Tanzania, linamshikilia, Emmaus Mwamakula, Askofu wa kanisa la Uamsho la Moravian kwa tuhuma za kuhamasisha maandamano nchi nzima yenye lengo la kudai katiba mpya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, aliyoitoa usiku wa tarehe 15 Februari 2021, imesema Askofu Mwamakula ametumia mitandao ya kijamii, kuhamasisha maandamano.

“Taarifa ilikuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi ili kuandamana wakishinikiza na kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi,” amesema Mambosasa

“Aidha awali, Jeshi la Polisi kupitia idara ya upelelezi kanda Maalum Dar es Salaam, walifanikiwa kupata taarifa hiyo na kumkamata Askofu huyo kwa ajili mahojiano kwa jambo hilo ambalo lilileta taharuki kwa umma katika mitandao ya kijamii.”

Mambosasa amesema “Jeshi la Polisi linatoa onyo kwa yeyote ambaye ameshawishika na kupanga kuandamana kuahirisha mara moja nia hiyo ovu ambayo iko kinyume na sheria.”

“Pia ifahamike ni kosa kufanya maandamano bila kuwa na kibali cha Polisi ili kupewa ulinzi, na atakayejaribu kuandamana atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria. Hivyo wananchi wote wa jiji la Dar es Salaam, waendelee na shughuli zao za kukuza uchumi na kujipatia vipato vyao vya kila siku,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!