Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Mwambusi aachana na Yanga
Michezo

Mwambusi aachana na Yanga

Juma Mwambusi, kocha msaidizi wa Yanga
Spread the love

KOCHA msaidizi wa timu wa Yanga, Juma Mwambusi ameamua kuachana na klabu hiyo mara baada ya kusumbuliwa na matatizo ya kiafya na kuhitaji kupumzika kwenye nafasi hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Akithitbitisha taarifa hiyo Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Mshindo Msolla amesema kuwa kocha huyo aliandika barua kwa uongozi kuomba kupumzika wakati timu ikiwa kwenye michuano ya kombe la mapinduzi visiwani Zanzibar mara baada ya kushauliwa na madaktari.

“Aliandika barua wiki mbili zilizopita kuomba apumzike baada ya kushauliwa na madaktari, na ameshauliwa akae nyumbani na hali ikitengemaa atarudi kwenye shughuli zake,” alisema Msolla.

Mwenyekiti huyo aliongezea kuwa mara baada ya kupokea barua hiyo watakaa na Mwalimu mkuu wa timu hiyo, Cedric Kaze kuona kama ataweza kufanya kazi hiyo peke yake mpaka Mwambusi atakapopona au atahitaji msaidizi mwingine.

“Kwa kifupi niseme anapumzika na sisi tutakaa na mwalimu tuone kama anaweza kufanya kazi hiyo mwenyewe au atataka msaidizi kwa hiyo tutamsikiliza,” aliongezea Msolla.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!