Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Michezo Mwambusi aachana na Yanga
Michezo

Mwambusi aachana na Yanga

Juma Mwambusi, kocha msaidizi wa Yanga
Spread the love

KOCHA msaidizi wa timu wa Yanga, Juma Mwambusi ameamua kuachana na klabu hiyo mara baada ya kusumbuliwa na matatizo ya kiafya na kuhitaji kupumzika kwenye nafasi hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Akithitbitisha taarifa hiyo Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Mshindo Msolla amesema kuwa kocha huyo aliandika barua kwa uongozi kuomba kupumzika wakati timu ikiwa kwenye michuano ya kombe la mapinduzi visiwani Zanzibar mara baada ya kushauliwa na madaktari.

“Aliandika barua wiki mbili zilizopita kuomba apumzike baada ya kushauliwa na madaktari, na ameshauliwa akae nyumbani na hali ikitengemaa atarudi kwenye shughuli zake,” alisema Msolla.

Mwenyekiti huyo aliongezea kuwa mara baada ya kupokea barua hiyo watakaa na Mwalimu mkuu wa timu hiyo, Cedric Kaze kuona kama ataweza kufanya kazi hiyo peke yake mpaka Mwambusi atakapopona au atahitaji msaidizi mwingine.

“Kwa kifupi niseme anapumzika na sisi tutakaa na mwalimu tuone kama anaweza kufanya kazi hiyo mwenyewe au atataka msaidizi kwa hiyo tutamsikiliza,” aliongezea Msolla.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!