Sunday , 26 March 2023
Home Kitengo Michezo Mwambusi aachana na Yanga
Michezo

Mwambusi aachana na Yanga

Juma Mwambusi, kocha msaidizi wa Yanga
Spread the love

KOCHA msaidizi wa timu wa Yanga, Juma Mwambusi ameamua kuachana na klabu hiyo mara baada ya kusumbuliwa na matatizo ya kiafya na kuhitaji kupumzika kwenye nafasi hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Akithitbitisha taarifa hiyo Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Mshindo Msolla amesema kuwa kocha huyo aliandika barua kwa uongozi kuomba kupumzika wakati timu ikiwa kwenye michuano ya kombe la mapinduzi visiwani Zanzibar mara baada ya kushauliwa na madaktari.

“Aliandika barua wiki mbili zilizopita kuomba apumzike baada ya kushauliwa na madaktari, na ameshauliwa akae nyumbani na hali ikitengemaa atarudi kwenye shughuli zake,” alisema Msolla.

Mwenyekiti huyo aliongezea kuwa mara baada ya kupokea barua hiyo watakaa na Mwalimu mkuu wa timu hiyo, Cedric Kaze kuona kama ataweza kufanya kazi hiyo peke yake mpaka Mwambusi atakapopona au atahitaji msaidizi mwingine.

“Kwa kifupi niseme anapumzika na sisi tutakaa na mwalimu tuone kama anaweza kufanya kazi hiyo mwenyewe au atataka msaidizi kwa hiyo tutamsikiliza,” aliongezea Msolla.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!