Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai kuwaapisha wabunge ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Spika Ndugai kuwaapisha wabunge ACT-Wazalendo

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai leo Jumanne tarehe 15 Desemba 2020, atawaapisha wabunge wanne wa ACT-Wazalendo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge imesema, wabunge hao wataapisha saa 10 jioni katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 27 na 28 Oktoba 2020, ACT-Wazalendo kilishinda majimbo manne ya Pemba visiwani Zanzibar.

Walioshinda ni; Hatibu Said Haji (Konde), Salum Mhamed Shafi (Chonga), Omar Ali Omar (Wete) na Khalifa Mhamed Issa wa Mtambwe.

Wabunge wateule wanakwenda kuapishwa baada ya chama hicho kuwaruhusu wanachama wake wote walioshinda udiwani, ubunge na uwakilishi kwenda vyombo vya uwakilishi ili kuapishwa na kuanza kuwatumikia wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

error: Content is protected !!