Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai kuwaapisha wabunge ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Spika Ndugai kuwaapisha wabunge ACT-Wazalendo

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai leo Jumanne tarehe 15 Desemba 2020, atawaapisha wabunge wanne wa ACT-Wazalendo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge imesema, wabunge hao wataapisha saa 10 jioni katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 27 na 28 Oktoba 2020, ACT-Wazalendo kilishinda majimbo manne ya Pemba visiwani Zanzibar.

Walioshinda ni; Hatibu Said Haji (Konde), Salum Mhamed Shafi (Chonga), Omar Ali Omar (Wete) na Khalifa Mhamed Issa wa Mtambwe.

Wabunge wateule wanakwenda kuapishwa baada ya chama hicho kuwaruhusu wanachama wake wote walioshinda udiwani, ubunge na uwakilishi kwenda vyombo vya uwakilishi ili kuapishwa na kuanza kuwatumikia wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!