Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwakilishi mteule ACT-Wazalendo afariki dunia
Habari za Siasa

Mwakilishi mteule ACT-Wazalendo afariki dunia

Spread the love

MWAKILISHI Mteule wa Pandani kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Abubakar Khamis Bakar (69) amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumatano tarehe 11 Novemba 2020, akiwa nyumbani kwake Mbweni visiwani Unguja, Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Katibu wa Idara ya Uenezi, Habari na Mawasiliano kwa Umma, Salim Bimani wakati anazungumza na MwanaHALISI Online kwa simu.

Bimani amesema, mwili wa Bakar aliyezaliwa tarehe 2 Novemba 1951 utazikwa jioni ya leo katika makaburi ya familia yake yaliyopo maeneo ya Kiyanga visiwani humo.

“Inaonekana alifariki nyumbani kwake Mbweni Unguja saa saba. Mazishi yatafanyika leo jioni katika makaburi ya familia yake maeneo ya Kiyanga,” amesema Bimani.

Kuhusu chanzo cha kifo hicho, Bimani amesema hadi sasa hakuna taarifa rasmi juu ya chanzo chake ila anahisi itakuwa ni shinikizo la moyo.

“Chanzo cha kifo chake hadi sasa hatujui rasmi kwa kuwa alikuwa mzima, nahisi alipata shinikizo la moyo,” amesema Bimani.

Awali, taarifa za kifo hicho zilitolewa na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Zitto amesema kifo hicho ni pigo kwa chama chake kwa kuwa marehemu Bakar alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya ACT-Wazalendo pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili.

“Kwa uchungu mkubwa. nawajulisha kuhusu msiba mkubwa tuliopata wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili Maalim Abubakar Khamis Bakar,” ameandika Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!