Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu aitisha maombi ya kitaifa
Habari za Siasa

Lissu aitisha maombi ya kitaifa

Spread the love

MGOMBEA Urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu ametoa wito kwa Watanzania wa dini zote kufanya maombi ya kitaifa Jumatatu ya tarehe 26 Oktoba 2020, ili kumuomba Mungu alivushe salama Taifa hilo katika Uchaguzi Mkuu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lissu ametoa ombi hilo leo Ijumaa tarehe 23 Oktoba 2020 kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Mgombea huyo wa Urais wa Chadema amewaomba Watanzania popote walipo waitumie siku hiyo kufanya maombi, dua na sala ili uchaguzi huo utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 uwe huru na wa haki.

“Watanzania wenzangu, hii ni wiki ya mwisho ya uchaguzi mkuu muhimu kuliko mwengine yoyote katika historia yetu, Jumatano ijayo mtaenda kupiga kura kuchagua viongozi. “

“Katika kipindi muhimu kama hiki, nawaomba Watanzania wenzangu wote, wa dini zote, tushirikiane kuiombea nchi yetu tuwe na uchaguzi huru, haki na unaokubalika na Watanzania wote na unaoeleweka na dunia yote ambayo sisi ni sehemu yake,” amesema Lissu.

Uchaguzi huo utahusisha wa madiwani, wabunge, wawakilishi upamnde wa Zanzibar pamoja na Marais wa Tanzania na Zanzibar

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

error: Content is protected !!