Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu aitisha maombi ya kitaifa
Habari za Siasa

Lissu aitisha maombi ya kitaifa

Spread the love

MGOMBEA Urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu ametoa wito kwa Watanzania wa dini zote kufanya maombi ya kitaifa Jumatatu ya tarehe 26 Oktoba 2020, ili kumuomba Mungu alivushe salama Taifa hilo katika Uchaguzi Mkuu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lissu ametoa ombi hilo leo Ijumaa tarehe 23 Oktoba 2020 kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Mgombea huyo wa Urais wa Chadema amewaomba Watanzania popote walipo waitumie siku hiyo kufanya maombi, dua na sala ili uchaguzi huo utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 uwe huru na wa haki.

“Watanzania wenzangu, hii ni wiki ya mwisho ya uchaguzi mkuu muhimu kuliko mwengine yoyote katika historia yetu, Jumatano ijayo mtaenda kupiga kura kuchagua viongozi. “

“Katika kipindi muhimu kama hiki, nawaomba Watanzania wenzangu wote, wa dini zote, tushirikiane kuiombea nchi yetu tuwe na uchaguzi huru, haki na unaokubalika na Watanzania wote na unaoeleweka na dunia yote ambayo sisi ni sehemu yake,” amesema Lissu.

Uchaguzi huo utahusisha wa madiwani, wabunge, wawakilishi upamnde wa Zanzibar pamoja na Marais wa Tanzania na Zanzibar

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!