Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkutano wa Lissu watawanywa kwa mabomu
Habari za Siasa

Mkutano wa Lissu watawanywa kwa mabomu

Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Lindi nchini Tanzania, limeutawanya kwa mabomu ya machozi, mkutano wa Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema aliokuwa anaufanya eneo la Somanga. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mkutano huo, umetawanywa leo Ijumaa tarehe 23 Oktoba 2020, wakati Lissu akiwa jukwaani ameanza kuwahutubia wananchi waliokuwa wamejitokeza kasikiliza.

Kabla ya kutawanya, Lissu alianza kuzungumza kwa kuwashukuru wana Somanga kwa kujitokeza ili kuwaelezea “ujumbe wa ilani ya Chadema ya uhuru, haki na maendeleo ya watu.”

Amesema, wakati wa kutafuta viongozi “ni wakati wa watu kuzungumza na kuzibana midomo.”

Lissu amesema, wamefika eneo hilo baada ya kuandika barua Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuelezea kuomba kufanya mkutano eneo hilo ambalo hakuna mgombea mwinmgine wa urais mkoani humo.

“Tumekuja hapa, lakini kuna watu wanataka kutuzuia, sisi tutazungumza, mwenye kuanzisha fujo aanzishe, mwenye kupiga watu na apige watu, ratiba ya uchaguzi na shughuli zote za mgombea urais, mamlaka inayohusika ni Tume ya Uchaguzi, si mtendaji wa kata, Rais au waziri mkuu,” alisema Lissu

Baada ya kauli hiyo, mabomu ya machozi yalifyatuliwa kuwatawanya wananchi huku Lissu mwenyewe akitulia jukwani, akiendelea kuona kinachoendelea na baadaye aliondoka jukwaani kwenda kwenye helikopita kwa ajili ya mikutano mingine mkoani humo.

Wakati akiondoka, alisikindizwa na wananchi waliokuwa wakiimba ‘rais, rais, rais…”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!