Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu, Magufuli kukutana Kigoma
Habari za Siasa

Lissu, Magufuli kukutana Kigoma

Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia chama kikuu cha upinzani nchini humo Chadema watakuwa Mkoa mmoja wa Kigoma na Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Wawili hao ambao wote ni wagombea urais wanakutana leo Jumamosi tarehe 19 Septemba 2020 kwa kila mmoja akiwa na shughuli yake.

Jana Ijumaa, Rais Magufuli ambaye ni mgombea urais kupitia Chama Chama Mapinduzi (CCM) alikuwa na mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

Lissu alifanya mikutano majimbo kadhaa ya Rukwa na Katavi.

Leo Jumamosi, ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inaonyesha Lissu atakuwa Mpanda Mjini mkoani katavi asubuhi kisha ataingia Kigoma akianza na Jimbo la Kigoma Kaskazini atakwenda Kalimi, Buhigwe na atamalizia mkutano Kigoma Mjini saa 10 jioni.

Ratiba hiyo hiyo inaonyesha, mgombea urais wa CCM, Rais John Magufuli Uvinza Mkoa wa Kigoma kisha ataingia Mkoa wa Tabora majimbo ya Kaliua na Urambo.

Hata hivyo, Rais Magufuli bado yuko mkoani Kigoma kwa shughuli ya kiserikali iliyoanza asubuhi kwa kumpokea Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye aliyefanya ziara ya siku moja.

Rais Ndayishimiye amewasilia Kigoma na kupokelewa na Rais Magufuli Uwanja wa Lake Tanganyika ambapo wamezungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza uwanjani hapo kisha kwenda kuzindua Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma na baadaye kwenda kuzungumza Ikulu ndogo mkoani humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

error: Content is protected !!