Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu, Magufuli kukutana Kigoma
Habari za Siasa

Lissu, Magufuli kukutana Kigoma

Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia chama kikuu cha upinzani nchini humo Chadema watakuwa Mkoa mmoja wa Kigoma na Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Wawili hao ambao wote ni wagombea urais wanakutana leo Jumamosi tarehe 19 Septemba 2020 kwa kila mmoja akiwa na shughuli yake.

Jana Ijumaa, Rais Magufuli ambaye ni mgombea urais kupitia Chama Chama Mapinduzi (CCM) alikuwa na mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

Lissu alifanya mikutano majimbo kadhaa ya Rukwa na Katavi.

Leo Jumamosi, ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inaonyesha Lissu atakuwa Mpanda Mjini mkoani katavi asubuhi kisha ataingia Kigoma akianza na Jimbo la Kigoma Kaskazini atakwenda Kalimi, Buhigwe na atamalizia mkutano Kigoma Mjini saa 10 jioni.

Ratiba hiyo hiyo inaonyesha, mgombea urais wa CCM, Rais John Magufuli Uvinza Mkoa wa Kigoma kisha ataingia Mkoa wa Tabora majimbo ya Kaliua na Urambo.

Hata hivyo, Rais Magufuli bado yuko mkoani Kigoma kwa shughuli ya kiserikali iliyoanza asubuhi kwa kumpokea Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye aliyefanya ziara ya siku moja.

Rais Ndayishimiye amewasilia Kigoma na kupokelewa na Rais Magufuli Uwanja wa Lake Tanganyika ambapo wamezungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza uwanjani hapo kisha kwenda kuzindua Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma na baadaye kwenda kuzungumza Ikulu ndogo mkoani humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!