Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Akifika kwetu, anaonesha ubaguzi
Habari za Siasa

Zitto: Akifika kwetu, anaonesha ubaguzi

Spread the love

AKIFIKA kwenye majimbo yanaoongozwa na wapinzani, anasema “mmechelewa kwa sababu mlichagua wapinzani.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Mafia … (endelea).

Ni kauli ya Zitto Kabwe, kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za ubunge kwenye Jimbo la Mafia tarehe 17 Septemba 2020.

Zitto ambaye  ni mgombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Mjini na Saed Kubenea, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo na mgombea ubunge wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam, ni miongoni mwa wanasiasa wa chama hicho waliohudhuria uzinduzi huo na kumnadi Riziki Shahali Ngwali anayegombea ubunge katika jimbo hilo.

Saed Kubenea

“Mfano; kuna mgombea mmoja wa urais, kila sehemu kuna mbunge wa upinzani anasema, hapa hakuna maendeleo sababu mmechagua upinzani au akienda sehemu anasema, mkichagua wapinzani hautapata maendeleo,” amesema Zitto bila kumtaja jina mgombea huyo.

Amesema, hoja hiyo siyo kwa kweli kwa kuwa, hata katika maeneo yanayongozwa na wabunge na madiwani kutoka chama tawala, yanaongoza kwa kukosa maendeleo.

Akikazia hoja hiyo, Zitto ametolea mfano Jimbo la Mafia ambalo halijawahi kuongozwa na mbunge kutoka vyama vya upinzani, halina maendeleo.

Zitto Kabwe

Kufuatia changamoto hiyo, Zitto amewashauri Watanzania kuchagua wagombea wa upinzani ili wapate mabadiliko ya uongozi yatakayochochea maendeleo.

“Changamoto kubwa Mafia haiendelei ni sababu mmeikumbatia CCM, toka mfumo wa vyama vingi umeanza hamjawahi kupata mbunge kutoka upinzani,  hamjawahi kupatachangamoto mpya. Wabunge wenu walewale,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!