Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Maonyesho uchimbaji madini yaanza Geita, GGML yadhamini
Habari Mchanganyiko

Maonyesho uchimbaji madini yaanza Geita, GGML yadhamini

Spread the love

MAONYESHO ya tatu ya teknolojia za uchimbaji madini mkoani Geita yanayofanyika kati ya tarehe 17 hadi 27 Septemba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita … (endelea). 

Mdhamini wa maonyesho hayo ni Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) ambayo imetoa Sh.200 milioni ili kugharamia usawazishaji eneo, mabanda 100 pamoja na umeme wa dharura (jenereta na mafuta yake) katika kipindi chote.

Maonyesho hayo ambayo yanafanyika katika viwanja vya Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji na Mauzo Nje ya Nchi (EPZA) Mjini Geita ambalo pia limejengwa na Kampuni ya GGML kupitia mpango wake wa huduma kwa jamii kwa gharama za Shilingi Milioni 800.

Maonyesho haya yatakutanisha kampuni za uchimbaji madini, wachimbaji wadogo na wa kati, wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Tanzania na nchi nyingine kwa ajili ya kuonyesha teknolojia zinazotumika katika sekta ya uchimbaji madini na fursa za uwekezaji na biashara kwenye sekta hiyo.

“GGML inajivunia kudhamini maonyesho haya kwa mwaka wa tatu mfululizo. Mwaka huu tunakusudia kutoa uzoefu wetu wa matumizi ya vifaa mbalimbali vya uchimbaji kwa kampuni nyingine lakini pia kwa wachimbaji wadogo,” alisema Simon Shayo, Makamu wa Rais wa GGML

“Tunajivunia kuendeleza ushirikiano na jamii inayotuzunguka kwa kunufaisha wafanyabiashara wa ndani wanaokusudia kufanya kazi na sisi,” alisema Shayo

alisema, anatarajia kuona ndoto ya kuwa na kituo cha uwekezaji na biashara ya nje mkoani jumo inatimia na GGML inakuwa sehemu ya mafanikio hayo kupitia mpango wake wa kusaidia jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!