Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Akifika kwetu, anaonesha ubaguzi
Habari za Siasa

Zitto: Akifika kwetu, anaonesha ubaguzi

Spread the love

AKIFIKA kwenye majimbo yanaoongozwa na wapinzani, anasema “mmechelewa kwa sababu mlichagua wapinzani.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Mafia … (endelea).

Ni kauli ya Zitto Kabwe, kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za ubunge kwenye Jimbo la Mafia tarehe 17 Septemba 2020.

Zitto ambaye  ni mgombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Mjini na Saed Kubenea, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo na mgombea ubunge wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam, ni miongoni mwa wanasiasa wa chama hicho waliohudhuria uzinduzi huo na kumnadi Riziki Shahali Ngwali anayegombea ubunge katika jimbo hilo.

Saed Kubenea

“Mfano; kuna mgombea mmoja wa urais, kila sehemu kuna mbunge wa upinzani anasema, hapa hakuna maendeleo sababu mmechagua upinzani au akienda sehemu anasema, mkichagua wapinzani hautapata maendeleo,” amesema Zitto bila kumtaja jina mgombea huyo.

Amesema, hoja hiyo siyo kwa kweli kwa kuwa, hata katika maeneo yanayongozwa na wabunge na madiwani kutoka chama tawala, yanaongoza kwa kukosa maendeleo.

Akikazia hoja hiyo, Zitto ametolea mfano Jimbo la Mafia ambalo halijawahi kuongozwa na mbunge kutoka vyama vya upinzani, halina maendeleo.

Zitto Kabwe

Kufuatia changamoto hiyo, Zitto amewashauri Watanzania kuchagua wagombea wa upinzani ili wapate mabadiliko ya uongozi yatakayochochea maendeleo.

“Changamoto kubwa Mafia haiendelei ni sababu mmeikumbatia CCM, toka mfumo wa vyama vingi umeanza hamjawahi kupata mbunge kutoka upinzani,  hamjawahi kupatachangamoto mpya. Wabunge wenu walewale,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!