Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Akifika kwetu, anaonesha ubaguzi
Habari za Siasa

Zitto: Akifika kwetu, anaonesha ubaguzi

Spread the love

AKIFIKA kwenye majimbo yanaoongozwa na wapinzani, anasema “mmechelewa kwa sababu mlichagua wapinzani.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Mafia … (endelea).

Ni kauli ya Zitto Kabwe, kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za ubunge kwenye Jimbo la Mafia tarehe 17 Septemba 2020.

Zitto ambaye  ni mgombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Mjini na Saed Kubenea, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo na mgombea ubunge wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam, ni miongoni mwa wanasiasa wa chama hicho waliohudhuria uzinduzi huo na kumnadi Riziki Shahali Ngwali anayegombea ubunge katika jimbo hilo.

Saed Kubenea

“Mfano; kuna mgombea mmoja wa urais, kila sehemu kuna mbunge wa upinzani anasema, hapa hakuna maendeleo sababu mmechagua upinzani au akienda sehemu anasema, mkichagua wapinzani hautapata maendeleo,” amesema Zitto bila kumtaja jina mgombea huyo.

Amesema, hoja hiyo siyo kwa kweli kwa kuwa, hata katika maeneo yanayongozwa na wabunge na madiwani kutoka chama tawala, yanaongoza kwa kukosa maendeleo.

Akikazia hoja hiyo, Zitto ametolea mfano Jimbo la Mafia ambalo halijawahi kuongozwa na mbunge kutoka vyama vya upinzani, halina maendeleo.

Zitto Kabwe

Kufuatia changamoto hiyo, Zitto amewashauri Watanzania kuchagua wagombea wa upinzani ili wapate mabadiliko ya uongozi yatakayochochea maendeleo.

“Changamoto kubwa Mafia haiendelei ni sababu mmeikumbatia CCM, toka mfumo wa vyama vingi umeanza hamjawahi kupata mbunge kutoka upinzani,  hamjawahi kupatachangamoto mpya. Wabunge wenu walewale,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!