Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga wazindua jezi mpya 2020/21
Michezo

Yanga wazindua jezi mpya 2020/21

Spread the love

MABINGWA wa kihistoria wa soka nchini Tanzania, Yanga ya jijini Dar es Salaam, wamezindua jezi mpya ambazo zitatumika katika msimu wa 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwapungu, Dar es Salaam … (endelea).

Uzinduzi huo umefanyikia makao makuu ya timu hiyo, Jangwani leo Ijumaa tarehe 11 Septemba, 2020 na kuhudhuriwa viongozi mbalimbali wa Yanga akiwemo Makamu Mwenyekiti wake, Fredrick Mwakalebela na Mshauri wa timu hiyo, Senzo Mazingisa.

Yanga imekuwa klabu ya kwanza Tanzania kuwa na duka lake la vifaa vya michezo katika makao ya timu ambapo, Senzo amewaomba mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kununua ili kuongeza mapato ya timu na kuifanya kuendelea kuwa bora zaidi ndani na nje ya Tanzania.

Senzo amesema huo ni mwelekeo mzuri wa timu kuwa na duka lake la vifaa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa GSM, Hersi Said amesema, kila mwaka watakuwa wanatengeneza jezi nzuri “hatutengenezi jezi tu bora tumetengeneza” na zitakuwa zinaendena na tamaduni za Kiafrika na ki-Yanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!